Monday, August 20, 2012

KUWANYIMA HAKI ZA MSINGI IDADI HII YA WATU SI SAWA

Zaidi ya watu milioni 34 wanaishi na virusi vya HIV.

Takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka 2011 zaidi ya watu milioni 34 ulimwenguni wanaishi na maambukizi ya Virusi vya ugonjwa wa Ukimwi (VVU) kati ya hao milioni 30.7 watu wazima, milioni 16.7 wanawake na milioni 3.4 watoto wenye umri wa chini ya miaka 15.
Hayo yamesemwa jana na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Kupambana na Ugonjwa wa Ukimwi (UNAIDS) Dkt. Raul de Melo Cabral wakati akiongea na wake wa wakuu wa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) waliohudhuria mkutano wa kuzuia maambukizi ya virusi vya Ugonjwa wa Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kwa maendeleo ya kanda unaofanyika Maputo nchini Msumbiji.
 Na Anna Nkinda – Maputo

No comments: