Wednesday, September 12, 2012

MAN ACCUSED OF SEX WITH BOY, 15, TRANSMITTING HIV

Keith Sumlin is HIV positive, police said

A 30-year-old Sunrise man was arrested Wednesday and charged with seven sex offenses involving a 15-year-old Pembroke Pines boy, police said.

The mother of the teenager called Pembroke Pines Police on Sunday when her son claimed Keith "Keyoko" Sumlin had sex with him in August.

The teenager told detectives he met Sumlin through a cell phone app. He told Sumlin he was under 18 and Sumlin claimed to be 21, police said.

When the teenager told a friend about the sex acts, the friend told him Sumlin was HIV positive. He said that Sumlin had sex with other young men and boys that he videotaped and posted online with a link to his Facebook page, according to the arrest report.

Preliminary medical checks have revealed that the suspect tested positive for the virus. A follow up also revealed the victim had tested positive, the report stated.

During questioning, Sumlin admitted to having sex with the 15-year-old but claimed he used a condom, police said.

Out of concern for public health and safety, investigators are urging anyone who may have had any interaction or relationship with Sumlin to contact Pembroke Pines Police at 954-436-3200.

Friday, 07 September 2012 14:16 Written by Wayne K. Roustan, Sun Sentinel

Thursday, September 6, 2012

FROM UNDP DESK...

Protecting the rights of people with HIV is essential for halting the spread of the epidemic...

INATISHA...

KILA DAKIKA MSICHANA MMOJA HUAMBUKIZWA VIRUSI VYA UKIMWI.....@UNAIDS.

Wednesday, September 5, 2012

UFADHILI

Tacaids kuacha kuwategemea wafadhili: TUME ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS ) inakusudia kuanzisha mfuko maalumu kwa ajili ya kuhudumia afya mbalimbali za Ukimwi ili kuondokana na utegemezi wa fedha za wafadhili na wahisani kutoka nje kwa ajili ya kuhudumia jambo hilo.

TACAIDS

TUME ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) imeeleza kuwa rushwa ya ngono sehemu za utumishi wa umma ni changamoto mpya, inayochangia kukwamisha juhudi za kupunguza maambukizi mapya ya Ukimwi nchini.

Mwenyekiti Mtendaji wa Tacaids, Dk Fatma Mrisho, alisema hayo mwanzoni mwa wiki hii kwenye warsha ya siku mbili iliyoshirikisha watendaji wakuu kutoka Idara za Utumishi wa Umma.

Kutokana na kukithiri kwa aina hiyo ya rushwa katika utumishi wa umma, alitaka waajiri na watu wengine wenye tabia hizo kuacha na wazingatie haki, sheria na vigezo wanapohitaji kuajiri watumishi wapya.

Dkt. Mrisho alibainisha, kwamba Tanzania imefanikiwa kupunguza maambukizi ya UKIMWI tangu mwaka 2004 kutoka asilimia saba na kufikia asilimia 5.7. Akizungumzia mafanikio machache ya mkakati wa kupunguza maambukizi, alisema kuwa asilimia 94 ya Watanzania hawana maambukizi na hivyo ni vyema kila mmoja kuendelea kujikinga. Kutokana na mwelekeo huo, aliomba wananchi waendelee kuchukua hadhari za kujikinga ili wasiambukizwe.

Monday, August 20, 2012

UMOJA WA MATAIFA

KUKUZA HAKI ZA BINADAMU


Tangu Baraza kuu lilipokubali. Haki za Binadamu Ulimwenguni miaka 1948, Umoja Wa

Mataifa umesaidia kufanya mikataba ya haki za kisiasa, kiraia, kiuchumi, kijamii na

kitamaduni, kuwa sheria shirika la UN la Haki za binadamu limefanya uchunguzi wa

malalamiko ya kibinafsi ya kesi ya mateso ulimwenguni, Kupotea na kuwekwa kizuizini

bila sababu na kufaulu kuhimiza serikali ulimenguni kuimarisha na kuboresha rekodi zao

za Haki za kibinadamu.

KUHUSU UBAGUZI....

Mtu yeyoye atakayekiuka sheria na


kufanya vitendo vya kibaguzi au unyanyapaa kama

vilivyokatazwa na sheria atakuwa amefanya kosa

kwa mujibu wa kifungu cha 32 cha sheria hii na

akipatikana na hatia atatozwa faini isiyopungua

shilingi za Tanzania milioni mbili au kifungo kisichozidi

mwaka mmoja au vyote kwa pamoja.

WAJIBU WA KILA MTU AU TAASISI KATIKA KUPAMBANA NA UKIMWI


Sheria hii inaweka wajibu kwa kila mtu anayeishi ndani ya Tanzania Bara, kila

kitengo kinachofanya kazi ndani ya Tanzania Bara, na kila shirika lililosajiliwa ndani

ya Tanzania Bara wa kufanya yafuatayo;

-Kuuambia umma na kuuelimisha juu ya vyanzo vya ugonjwa wa UKIMWI, jinsi

maambukizi yanavyotokea, madhara yake na jinsi ya kudhibiti maambukizi

ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI.

- Kupunguza kuenea kwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI.

- Kupunguza uwepo wa magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya ngono

zembe katika jamii.

- Kupunguza madhara yanayosababishwa na virusi vya UKIMWI na UKIMWI.

-Kulinda haki za watoto yatima kwa kufanya yafuatayo:

i. Kuwapatia huduma za afya na za kijamii;

ii. Kukataza upimaji wa virusi vya UKIMWI kwa lazima labda kama

ulazima huo ni kwa mujibu wa sheria; na

iii. Kupinga unyanyapaa na ubaguzi kwa waathirika wa Virusi wa

UKIMWI.

-Kupinga mila potofu ambazo zinachangia maambukizi ya UKIMWI na virusi

vya UKIMWI katika jamii.

- Kutetea na kuendeleza mila zote nzuri ambazo husaidia kupunguza

maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI katika jamii.

- Kuwasaidia watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI na UKIMWI kupata

ushirikiano wa kutosha kutoka katika jamii hasa kwa kuwawezesha kufikia

huduma za afya.

SHERIA ZA TANZANIA DHIDI YA HAKI ZA WATU WAISHIO NA UKIMWI

Sheria zilizopo na inayopendekezwa kwa sasa na serikali ya Tanzania kwa ajili ya kulinda na kusimamia haki za wenye UKIMWI zinatakiwa zilenge au zijikite katika UTAWALA WA SHERIA.Utawala wa sheria hapa namaanisha kusimamia demokrasia katika idara zote, Kuhakikisha uwazi na ukweli katika kutekeleza haki kwa sababu ya usemi usemao(justice should not be done but also should be seen to be done) haki sio tu ifanyike bali pia ionekane ikifanyika, kujiepusha na rushwa, na kuwepo na sheria itakayo kuwa rahisi kutekelezeka na kufanyika.Serikali na viongozi wa siasa wanatakiwa Kuhakikisha haki za watu wenye ukimwi zinalindwa na kuheshimiwa. Uimara, uhuru, na usahihi wa bunge, mahakama, na idara mbalimbali za utawala ni muhimu katika jamii yenye democrasia ya kweli kama vile Tanzania.Sheria ya ukimwi itanufaisha walengwa na wananchi kwa ujumla na kukuza huduma za afya na malengo mengine kama yalivyo tajwa katika Sera ya UKIMWI ya 2001itategemea moja kwa moja etekelezaji wa sheria hiyo.

Mswada wa sheri wa kusimamia haki za msingi za binadamu iliiingizwa katika katiba ya Tanzania mnamo mwaka 1984 na sheria inayolinda haki hizo ni (constitution(fifth)amendment) ACT, 1984 Act no.15 ya mwaka 1984 imetaja mikakati ya kupinga kutengwa kwa watu hawa waishio na UKIMWI katika ibara za katiba yetu hii hasa ibara ya 12 mpaka ya 29.Tutazijadili ibara hizi kwa kina siku nyingine.

Pamoja na hayo, mambo ambayo nitayajadili hapa ni utekelezwaji wa haki hizo zilizopo ndani ya katiba yetu hii,ili zitosheleze kuwalinda watu waishio na UKIMWI ili kuepekana na Kutengwa na kubaguliwa katika jamii na sekta nyingine za umma.

Tanzania, kubagua na kunyanyapaa kunaonekana katika sehemu mbali mbali kama vile, katika ngazi ya familia, vyombo vya habari, sehemu za kazi, idara ya elimu, idara ya afya, na dini pia. Unyanyapaa na kubagua dhidi ya watu waishio na UKIMWI kunasababisha jitihada za kuzuia na kupambana na UKIMWI kuwa ngumu.

Nchini hapa(Tanzania) kuna zana na njia mbalimbali za kisheria ambazo zipo kwa ajili ya kulinda uvunjaji wa haki za binadamu zilizo hakikishwa ndani ya katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Miongoni mwa njia zitumikazo ni bunge kubadili sheria mbalimbali kwa mfano;

Sheria ya mashtaka dhidi ya serikali(government proceeding Act) 1967 ambayo kabla ilikuwa ikimtaka mtu kupata idhini ya mwanasheria mkuu ili aishitaki serikali hata kama imefanya kosa kubwa kabisa la uvunjaji wa haki za binadamu.Baada ya kubadilishwa sasa mtu anaweza kuishtaki serikali baada tu ya kuitumia notisi ya siku 90 kuonyesha dhamira yake ya kutaka kuishtaki.Sheria nyingine ni ( BASIC RIGHTS AND DUTIES ENFORCEMENT ACT NO.33 1994)

Sheria hii ya utekelezaji wa haki na wajibu ya mwaka 1994(BASIC RIGHTS AND ENFORCEMENT ACT 1994), ni sheria itoayo utaratibu wa utekelezaji wa haki za msingi zilizotolewa ndani ya katiba na mambo mengine kama hayo. Kwa hiyo mtu yeyote ambae anadai kuwa moja wapo ya ibara ya 12 mpaka 29 ya katiba imevunjwa au inaelekea kuvunjwa anaweza kuomba au kufungua mashtaka mahakama kuu ya Tanzania kw ajili ya kupata haki zake. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha sheria hii.

Kifungu cha 13 cha sheria hii, kinasema pamoja na mambo mengine kama mahakama kuu itaona kuwa ni kweli haki za mtu huyo zimevunjwa itakuwa na nguvu ya kuamuru haki hizo kutekelezwa juu ya mtu huyo kama zilivyo tolewa katika ibara ya 12 mpaka ya 29.

PAMOJA NA HAYO, Utekelezwaji na usimamizi wa vifungu hivi katika sheria hii haupo kivitendo. Hii ni kwa sababu zifuatazo:

Kwanza, sheria hii ndani yake kuna ibara ya 10 ambayo inasema katika utoaji wa haki hizi panatakiwa kuwepo na majaji watatu kusikiliza madai hayo badala ya jaji mmoja.
Kwa Tanzania ni vigumu kuwa na majaji watatu katika kikao kimoja kwa sababu ya ukosefu wa majaji nchini kwetu, hiki ni kipingamizi kwa kuwa watu huona kesi zao zitachukua mlolongo mrefu mahakamani katika kusubiri hadi majaji watatu wakae.

Kwa kifupi kifungu cha 10 na 13 cha sheria hii ya mwaka 1994 kinatakiwa kitazamwe upya kama kweli tunataka kupambana na ugonjwa huu na haki za watu hawa kwa ujumla kwa kuwa vifungu hivi kwa ujumla wake havitoi nafasi kwa watu waishio na ukimwi kuzipata haki zao za msingi.

NITAENDELEA KUZIJADILI SHERIA NYINGINE ZINAZO ONYESHA UWEZEKANO WA KUWABAGUWA NA KUWANYANYAPAA WENYE UKIMWI.

KUWANYIMA HAKI ZA MSINGI IDADI HII YA WATU SI SAWA

Zaidi ya watu milioni 34 wanaishi na virusi vya HIV.

Takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka 2011 zaidi ya watu milioni 34 ulimwenguni wanaishi na maambukizi ya Virusi vya ugonjwa wa Ukimwi (VVU) kati ya hao milioni 30.7 watu wazima, milioni 16.7 wanawake na milioni 3.4 watoto wenye umri wa chini ya miaka 15.
Hayo yamesemwa jana na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Kupambana na Ugonjwa wa Ukimwi (UNAIDS) Dkt. Raul de Melo Cabral wakati akiongea na wake wa wakuu wa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) waliohudhuria mkutano wa kuzuia maambukizi ya virusi vya Ugonjwa wa Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kwa maendeleo ya kanda unaofanyika Maputo nchini Msumbiji.
 Na Anna Nkinda – Maputo

HATUA NZURI SANA

Wake wa marais wa Afrika wasaini azimio la kupunguza VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

HAKI ZA WAISHIO NA UKIMWI

HAKI ni suala muhimu kwa kila mwanadamu, kwani hutumika kukulinda kisheria.Katika miaka ya nyuma hali ilikuwa ni mbaya kutokana na suala la Ukimwi na VVU kuwa ni suala geni sana machoni na masikioni mwa jamii, hususani linapojitokeza suala la kutanabaishwa jinsi ugonjwa huo ulivyo kuanzia sababu za kuupata, dalili hadi njia za kuuzuia au matibabu.
1.  Haki ya kutobaguliwa.Kubaguliwa ni haki muhimu ambayo huweza kusababisha madhara kama ya kufikia hatua ya mhusika kuchukua hatua mbaya iwapo atakuwa akibaguliwa na jamii inayomzunguka.
2. Haki ya kupata taarifa sahihi,Kwa kiasi kikubwa hili ni tatizo lililopo ndani ya jamii kiujumla sio tu kwa wale waishio na VVU na Ukimwi tu bali hata kwa wale wenye matatizo ya aina nyingine.
Mara nyingi tumeweza kuona makosa mbalimbali ambayo baadhi ya wataalamu kama vile madaktari walivyokosea na kutoa taarifa zisizo sahihi hali iliyosababisha labda kifo au hata madhara makubwa kwa ndugu jamaa na marafiki zetu.
Kwa maana hiyo jambo muhimu ni kufahamu kuwa haki ya kupata taarifa sahihi iwapo kama ni majibu ya tatizo alilonalo baada ya kupima, kuwa hiyo ni haki yake ya kimsingi ambayo inatakiwa kutekelezwa kwa makini sana ili taarifa zake zisije potoshwa na baadae kusababisha madhara.


NIKWELI TUNAHITAJI KUWA NA HARAKATI ZA HAKI ZA BINADAMU KIPINDI HIKI KULIKO WAKATI MWINGINE WOWOTE?

NITABAKIA KUWA BINADAMU HATA KAMA NINAISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI

.

Sunday, August 19, 2012

EID MUBARAK

Sikukuu njema, nawatakia kila la kheri na uangalifu mkubwa katika kipindi hiki cha sikukuu ya Eid el fitr....

Friday, August 17, 2012

SERIKALI INATAKIWA KUJIINGIZA MOJA KWA MOJA KATIKA MAPAMBANO HAYA

“The government must review its policies to ensure that the sexual and reproductive health of women living with HIV is protected, including issuing clear guidelines for informed consent for sterilization and legal abortion.”

Tuesday, August 14, 2012

MBAYA SANA HII....TUPAMBANE PAMOJA?

.

HALI HALISI NDIO HII....

UKIMWI SASA SIO JANGA LA KITAIFA



Sunday, 12 August 2012 00:21

UGONJWA wa Ukimwi hautakuwa tena janga la kitaifa nchini miaka michache ijayo baada ya Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids) kueleza kuwa Tanzania imekusudia kubadili sera na mikakati ya kukabili ugonjwa huo.



Mkurugenzi wa Sera, Mipango na Utafiti wa Tacaids, Dk Raphael Kalinga aliliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam mapema wiki hii kuwa, chini ya mkakati huo Ukimwi utakuwa ni tatizo la mtu binafsi na makundi maalumu.



Mpango huo unafuatia matokeo ya Mkutano wa Kimataifa wa Ukimwi uliofanyika nchini Marekani hivi karibuni na kujifunza juu ya maendeleo ya kisayansi ya kudhibiti Ukimwi ambao ujumbe wa Tacaids ulihudhuria akiwamo Dk Kalinga.



"Awali tulikuwa tunakubaliana kuwa, ‘Ukimwi ni janga la Kitaifa’. Kwa maana kwamba tulikuwa tunaenda na population yote (idadi ya watu nchi nzima)," alisema Dk Kalinga kwenye mahojiano na Mwananchi Jumapili mapema wiki hii, baada ya kurejea nchini kutoka Marekani.



Alisema kuwa, sera hiyo ya kizamani na kwamba sasa wataachana nayo na inawapasa kubadilika kulingana na tafiti za kisayansi, maendeleo na uzoefu uliothibitishwa kitaalamu.



Dk Kalinga alisema kuwa, mkakati ambao Tanzania itautumia ni wa kuuona Ukimwi kama janga la mtu binafsi na makundi maalumu yaliyo kwenye mazingira hatarishi.



"Kwa kutumia mbinu zenye kuleta matunda mazuri, tumeingia kwenye ubunifu mpya. Hatuutazami tena (Ukimwi) kama janga la kitaifa. Tunalitazama kama ni janga langu, au janga lako," alisema Dk Kalinga na kuainisha:



“Mtazamo wa Tacaids sasa ni kujikita zaidi kwenye makundi ya watu maalumu walio kwenye mazingira hatarishi, kama vile wanaofanya kazi migodini, wafungwa, wanaoendesha biashara ya kuuza miili yao na watumia dawa za kulevya.”



Dk Kalinga alisema kuwa, tatizo la Virusi Vya Ukimwi (VVU) ni la mtu binafsi.



Hata hivyo, alisisitiza kuwa, kila mtu anapaswa kufahamu kwamba Ukimwi ni tatizo hadi hapo itakapopatikana dawa ya chanjo au tiba iliyothibitishwa na mamlaka zinazotambulika duniani.



Dk Kalinga alibainisha kuwa, pamoja na kuwapo na dawa zinazozuia maambukizo, hata kutumika kama tiba, bado kila mtu atapaswa kuendelea kutumia elimu ya kukabiliana na VVU.



Alifahamisha elimu hiyo kuwa, ni pamoja na matumizi ya kondomu, wanaume kutahiriwa, kutibu mapema magonjwa ya zinaa, kuwa na mazoea ya kupima na kujua hali ya kiafya, kuzuia maambukizo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, ushauri nasaha, damu salama na matumizi sahihi ya dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV).



Dk Kalinga alisema pia kwamba wanatarajia kufanya kikao kitakachojumuisha wataalamu wa afya, watunga sera na wadau wa mapambano ya VVU nchini.



Kuhusu mkutano wa kukabiliana na Ukimwi uliofanyika Washington alisema kuwa, kimsingi katika mkutano huo uliomalizika Julai 27, mwaka huu waliazimia mkakati wa kuhakikisha kuwa hakuna unyanyapaa, kufa, kuambukiza ya VVU.



"Mkakati wetu ni kuwa na unyanyapaa sifuri, vifo sifuri na maambukizo sifuri," alisema Dk Kalinga ambaye pia ni mmoja wa wataalamu wa utafiti wa magonjwa ya binadamu nchini.



Mkutano huo ulikuwa wa kwanza kutamka kuwa VVU vinaweza kuangamizwa kabisa duniani.



Chini ya kauli ya kutokuwa na dawa wala chanjo, mkutano huo umeufumbua macho ulimwengu kwa kueleza kuwa zipo dawa zinazozuia mtu kuambukizwa Ukimwi, kuambukiza na kutibu.



Alipoulizwa nafasi ya Tanzania kufaidika na maendeleo hayo, Dk kalinga alisema pamoja na maendeleo hayo, nchi tajiri zina nafasi kubwa ya kufaidika zaidi zikilinganishwa na nchi maskini kama Tanzania.



Alisema katika nchi zilizoendelea, kama Marekani, watu wake wako katika nafasi nzuri zaidi ya kutumia dawa maalumu zinazozuia kuambukizwa VVU kutokana na mazingira yake ya elimu, ubora wa huduma za afya, uwezo wa kifedha na urahisi wa mawasiliano.



Hata hivyo, Dk Kalinga alibainisha kuwa hatari ya dawa hiyo kutumika katika nchi maskini kuwa ni kusababisha usugu wa maradhi hayo kwa sababu watu ambao hawajajichunguza kikamilifu kama wameambukizwa VVU wanaweza kuitumia.



Alisema kitaalamu dawa hiyo inapaswa kutumiwa na mtu asiye kabisa na virusi mwilini.



Hata hivyo, alisema kwa mazingira ya nchi maskini, ARV zina nafasi ya kusaidia kuzuia maambukizo ya Ukimwi, hata kutibu na kumfanya mwathirika aweze kuishi bila matatizo makubwa ya kiafya.



"Dawa za kuzuia kuambukizwa zikiletwa hapa wengi wataanza kuzitumia bila kujua hali zao kama wameambukizwa. Tuna uzoefu wa watu wetu, wanaweza wakadharau kwenda kupima na kusema: 'acha tu nimeze, itajulikana tu huku mbele', jambo ambali kiafya ni hatari," alionya Dk Kalinga.



Alisema mkutano huo kuhusu Ukimwi uliomalizika nchini Marekani umekuwa ukifanyika kila baada ya miaka miwili kwa kuwakutanisha wanasayansi, watunga sera na wadau wa mapambano ya VVU kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujifunza mbinu mpya na kuoana namna bora ya kupata fedha za kukabili tatizo hilo dunia nzima.



Maazimio ya mkutano

Jumamosi iliyopita, gazeti la Mwananchi liliripoti kuhusu mkutano huo uliomalizika kwa wajumbe zaidi ya 20,000 kuridhia maendeleo ya kisayansi yaliyofikiwa kwa sasa, wakisema ni madhubuti hivyo kutoa azimio la kuungana kuangamiza janga la maradhi hayo duniani.



Moja ya maazimio yao ni kuifikisha dunia mahali ambapo hakutakuwa na mtu atakayekufa, wala atakayekuwa akiishi na VVU.



Hii inatokana na matumaini ya kisayansi waliyohakikishiwa na watafiti juu ya kuwepo kwa dawa zinazoweza kuzuia maambukizo mapya na ambazo zikitumika kikamilifu zinaweza kufanya kazi kama tiba.



Pamoja na kuwapo kwa dawa hizo, walikiri kuwa mkakati huo hauwezi kufikiwa iwapo dunia haitajenga mshikamano wa pamoja wa kisera, uelimishaji na fedha za kutosha kufanikisha mbinu hizo mpya za kisayansi.



Rais wa Taasisi ya Kijamii ya Kimataifa ya Mapambano dhidi ya VVU (IAS), Dk Elly Katabira alisema kuna mambo mengi yaliyothibitishwa kisayansi huko nyuma, lakini kwa kuwa hakukuwa na mikakati madhubuti, tatizo hilo limeendelea kuwa janga la dunia.



Dk Katabira ambaye pia ni mmoja wa watafiti wa kisayansi katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Makerere, Uganda alitoa mfano wa watoto kuendelea kuambukizwa Ukimwi wanapozaliwa wakati tayari dawa ya kuondoa tatizo hilo ipo.



FURAHA...........

HII NI SAWA KABISA....

NIKWELI KABISA KABISA HATA KAMA ATAKUWAJE, BINADAMU ANABAKIA NA HAKI ZAKE ZA ASILI.

NIKWELI KABISA KABISA HATA KAMA ATAKUWAJE, BINADAMU ANABAKIA NA HAKI ZAKE ZA ASILI.

NIKWELI KABISA KABISA HATA KAMA ATAKUWAJE, BINADAMU ANABAKIA NA HAKI ZAKE ZA ASILI.

NIKWELI KABISA KABISA HATA KAMA ATAKUWAJE, BINADAMU ANABAKIA NA HAKI ZAKE ZA ASILI.

NIKWELI KABISA KABISA HATA KAMA ATAKUWAJE, BINADAMU ANABAKIA NA HAKI ZAKE ZA ASILI.

TUNAICHUKULIAJE HII?

ITAPUNGUZA SANA TU..TUJARIBU.....

Maswali ya kujiuliza wadau...

1. Je ni muhimu mtu kuwa na maandishi yanayothibitisha nia ya kutaka kupima HIV?
2. Je hospitali inaweza kumpima mtu bila hiari yake?
3. Je hospitali ikiandika kwamba inawapima wagonjwa wake UKIMWI inamaanisha wagonjwa wake wote watakaotembelea pale wamehiari kupima?
4. Je dokta anatakiwa kufanya siri ya majibu ya mgonjwa kwa staff(nurses)?

Tuzungumze mapambano ya kweli

Dadhani bado kuna udhaifu mkubwa katika mapambano haya ya ukimwi hasa kwa kuzingatia haki za binadamu kwa waishio na ukimwi....

Saturday, August 11, 2012

Hivi tunaweza kupambana na maambukizi ya ukimwi bila kuhusisha na suala zima la haki za binadamu?

UKIMWI NI WETU SOTE,WANAO ISHI NA UKIMWI NI NDUGU ZETU,TUSIWANYAPAE NA WALA TUSIWATENGE.

Friday, October 14, 2011

Tupige vita UNYANYAPAA MIAKA 50 MINGINE IJAYO



Inatakiwa kuwa hivi kua na UKIMWI haimaanishi ndio mwisho wa maisha....